Yanga kazi ndo kwanza imeanza.Lakini msitishike sana na hii timu pia lakini msijiamini sana eti kwa kuwa mna usajili wa bei mabaya!Usajili wenu kwa timukama ya Waarabu hawa wao pesa ya wachezaji wenu wote mlioitumia kwenye usajili wao ni ya kununulia mchezajimmoja tu Flavio wa Angola! Muhimu hapa ni kujitambua na kujielewa pia kufahamu kuwa lazima mfanye maandalizi ya maana toka sasa ili kuwezakukabiliana nao hawa jamaa.Maandalizi yawe ya maana na wala si ya zima moto.Mfanye maandalizi kwelikweli na wala si mchezo na wala si vinginevyo!.Najua ni vigumu kuyatekeleza mambo yote mawili yaani kuacha woga mbele ya hawa jamaa na pia kujiamini kupita kiasi mbele ya hawa jamaa.Lakini mkiyatafakari haya kwa kina basi mtawezakujielewa ni jinsi gani mikakati yenu mtakavyoipanga kuwezakuwakabili Waarabu hawa.Lakini suala la kufungika kwa hawa jamaa ni kitu kinachowezekena kabisa iwapo mtaamua.Lakini ninyi wachezaji mkishikamana na kocha wenu nina hakika mnaweza.Hakika mimi nina hakika mnaweza.
Ushauri wangu kwenu ni huu.Najua kuwa viongozi wenu karibu wote ni waoga na lazima watakuwa na mchecheto sana wa kupambana na Waarabu wale.Cha muhimu wala msiwasikilize,bali ninyi jinsi mnavyojiamini ni hivyo mtakavyoweza kuwafunga Waarabu wale.Kuanzia sasa jitumeni sana mafunzo na mazoezi ya mwalimu na lazima mjione kuwa mnaweza.Viongozi wenu kama nilivyosemani waoga.Watakuja na visingizio kibao ili hata mkipoteza mechi muonekane kuwa ninyi si lolote kwa waarabu wale. Kuwa mbona eti imezoeleka siku zote ninyi ni wateja kwao la hasha hilo likataeni safari hii kwa kuwaonyesha kuwamnaweza!Sasa basi lazima hapamuwaumbue viongozi ingawa najua kuwa mwisho wa siku baada ya ushindi watakuja na majigambo mengi ya kuwa ohoo hii ndo Yanga Afrika bwana tumeshikamana tumekuwa kitu kimoja tumeshinda.Nawahakikishia kuwa kama mtashinda mjue wazi kuwa ushindi huo utakuwa umetokana na juhudi zenu ninyi kama wachezaji na si vinginevyo.Hapa nasisitiza tena kuwa viongozi wenu tayari wamekwishaanza kuiogopa hiyo mechi ,lakini kwa jinsi ninavyokiona kikosi chenu hakika kama mtaamua ninyi wenyewe kweli kabisa mnaweza!Yanga wakati ndiyo huu.Waonesheni Watanzania na wapenda soka kwa ujumla kuwa mnaweza!Wakati ndiyo huu!Kila laheri DarYanga Afrika wawakilishi pekee wa Tanzania mliosalia mashindanoni.
Monday, February 16, 2009
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment