Friday, February 20, 2009

KILA LAHERI TAIFA STARS IVORY COAST.

Taifa Stars,sisi Watanzania wote tupo pamoja nanyi katika safari yenu ya kuliwania kombe la Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za ndani.Tunawaombea kila laheri ili muweze kuliwakilisha vema Taifa letu katika michuano hiyo mipya kabisa katika medani ya soka katika Afrika.Tulio wengi tunaamini kuwa mnaweza maana mpaka kufika hatua hiyo kwa kweli safari ilikuwa ndefu sana.
Kitu muhimu tunachowakumbusha watanzania wenzetu ni kuwa kwa kweli lazima muelewe kuwa huko mmekwenda kuwakilisha Taifa hivyo kwa njia moja au nyingine mko vitani ingawa si vita vya vifaru na mizinga bali vitavya mchezo wa soka lakini hiyo ni vita.Jitahidini kadri ya uwezo wenu mpambane kadri ya ujuzi wenu wote mliopewa na mwalimu na huku mkijua kuwa watanzania wote wapo nyuma yenu.
Kitu muhimu ni ushindi ingawa tupo tayari kuyapokea matokeo yoyote yale.
TUNA UHAKIKA KUWA MNAWEZA MAANA MPAKA KUFIKIA HAPO MLIPO KAMA NILIVYOKWISHA SEMA NI KUW MMEONYESHA KUW NINYI MU WAZURI KAMA HAO WENGINE!
Nahodha Nsajigwa hakikisha kuwa timu yako chini ya uongozi wako ndani ya kiwanja inakuwa na nidhamu wakati wote wa mchezo!Kubishana na waamuzi bila sababu ya msingi hakutaweza kutusaidia hasa ikizingatiwa kuw waamuzi wao ndiyo watoa maamuzi ya mwisho hata kama wachezaji hawakubaliani nayo.Nimekutaja nahodha kuwa unawajibika kuongoza nidhamu hasa tukumbukapo matukio ya nyuma pale tunapolalamika hata kama mwamuzi amepotoka lakini hkuna sababu ya kubishana naye sana kwani matokeo yake ni kadi na hiyo itapunguza ngu ya timu ingawaje wakayi mwingine inakuwa kichocheo cha timu kupigana kwa nguvu hadi mwisho baada ya kuijikuta kuwa tupo pungufu.Tuache hasira tuzingatie nidhamu tuwe na umoja tucheze kwa pamoja kama timu kama msemo wetu wa kiswahili usemavyo kuw umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu!
Tuna hakika kuwa viongozi wenu wamewaeleza na kuwajulisha majukumu yenu na mipaka yenu.
Hakika STARS KAMA MKIAMUA NA NINADHANI HIVYO KUWA MUMEAMUA BASI MTAWEZA NA INSHALAH KOMBE LITATUA KATIKA ARDHI HII YA BONGO!BRAVO TAIFA STARS ALUTA KONTINUA!TUPO PAMOJA NANYI.MUNGU IBARIKI TANZANIA MUNGU IBARIKI TAIFA STARS.

Monday, February 16, 2009

YANGA AFRIKA MKIAMUA MNAWEZA KULIANGUSHA KABATI!

Yanga kazi ndo kwanza imeanza.Lakini msitishike sana na hii timu pia lakini msijiamini sana eti kwa kuwa mna usajili wa bei mabaya!Usajili wenu kwa timukama ya Waarabu hawa wao pesa ya wachezaji wenu wote mlioitumia kwenye usajili wao ni ya kununulia mchezajimmoja tu Flavio wa Angola! Muhimu hapa ni kujitambua na kujielewa pia kufahamu kuwa lazima mfanye maandalizi ya maana toka sasa ili kuwezakukabiliana nao hawa jamaa.Maandalizi yawe ya maana na wala si ya zima moto.Mfanye maandalizi kwelikweli na wala si mchezo na wala si vinginevyo!.Najua ni vigumu kuyatekeleza mambo yote mawili yaani kuacha woga mbele ya hawa jamaa na pia kujiamini kupita kiasi mbele ya hawa jamaa.Lakini mkiyatafakari haya kwa kina basi mtawezakujielewa ni jinsi gani mikakati yenu mtakavyoipanga kuwezakuwakabili Waarabu hawa.Lakini suala la kufungika kwa hawa jamaa ni kitu kinachowezekena kabisa iwapo mtaamua.Lakini ninyi wachezaji mkishikamana na kocha wenu nina hakika mnaweza.Hakika mimi nina hakika mnaweza.
Ushauri wangu kwenu ni huu.Najua kuwa viongozi wenu karibu wote ni waoga na lazima watakuwa na mchecheto sana wa kupambana na Waarabu wale.Cha muhimu wala msiwasikilize,bali ninyi jinsi mnavyojiamini ni hivyo mtakavyoweza kuwafunga Waarabu wale.Kuanzia sasa jitumeni sana mafunzo na mazoezi ya mwalimu na lazima mjione kuwa mnaweza.Viongozi wenu kama nilivyosemani waoga.Watakuja na visingizio kibao ili hata mkipoteza mechi muonekane kuwa ninyi si lolote kwa waarabu wale. Kuwa mbona eti imezoeleka siku zote ninyi ni wateja kwao la hasha hilo likataeni safari hii kwa kuwaonyesha kuwamnaweza!Sasa basi lazima hapamuwaumbue viongozi ingawa najua kuwa mwisho wa siku baada ya ushindi watakuja na majigambo mengi ya kuwa ohoo hii ndo Yanga Afrika bwana tumeshikamana tumekuwa kitu kimoja tumeshinda.Nawahakikishia kuwa kama mtashinda mjue wazi kuwa ushindi huo utakuwa umetokana na juhudi zenu ninyi kama wachezaji na si vinginevyo.Hapa nasisitiza tena kuwa viongozi wenu tayari wamekwishaanza kuiogopa hiyo mechi ,lakini kwa jinsi ninavyokiona kikosi chenu hakika kama mtaamua ninyi wenyewe kweli kabisa mnaweza!Yanga wakati ndiyo huu.Waonesheni Watanzania na wapenda soka kwa ujumla kuwa mnaweza!Wakati ndiyo huu!Kila laheri DarYanga Afrika wawakilishi pekee wa Tanzania mliosalia mashindanoni.

Friday, February 06, 2009

JE TUMEMUELEWA MAMA ANNA TIBAIJUKA?

Kwa waliongalia kipindi cha TV cha Chanel Ten kinachojulikana kama "Je Tutafika kinachoendeshwa na mzee wetu Makwaia Wa Kuhenga akimhoji mama Tibaijuka kuhusu mauaji ya Maalbino nchini mwetu,sijui kama Watanzania wenzangu tulimuelewa vizuri yule mama wa Kitanzania msomi aliyebobea na mwenye kuheshimika sana Kimataifa.Napenda kumpongeza mama kwa jinsi alivyoweza kuisaidia jamii ya Watanzania kupitia kipindi kile ni kwa namna gani tutaweza kuzuia mauaji ya ndugu zetu Maalbino wasio na hatia.

Ameongea mambo ambayo hakuna hata mmoja wetu kuwa aliwahi kuwaza hata siku moja kuwa je ni njia gani tuweze kutafuta ilituweze kuzuia mauaji hayo?

Sina ya kuongea mengi lakini kama Chanel Ten wataweza kukirudia kile kipindi mara kwa mara ili Watawala wetu na Watanzania kwa ujumla tuweze kupata somo alilotoa yule mama wa Muleba ambaye anaishi na kuutumikia ulimwengu huu huko New York.

Mama Hongera sana kwa kweli umenikuna sana na nilikuelewa sana sana.Hakika tunatakiwa tuache kabisa kile ulichokiita kuwa "Stroke Brush Conclutions" kama sijakosea.Na pia kuwa kama ulivyosema kuwa lazima mtu anaposema kuwa amefanya utafiti basi uwe utafiti na si vinginevyo!

Mama somo lile ni la maana sana.Wasiwasi wangu je tumelielewa?Tujitahidi kwa bidii na maarifa tulielewe somo lile!Mzee Makwaia hongera kwa mumleta mama Anna kututatulia ili tupate ufumbuzi wa kuwakomesha hawa washenzi wasiostaraabika kwa kufikiri mawazo ya kipumbavu kuwa utajiri utatokana na viungo vya binadamu wenzetu Maalbino.Narudia tena kama tutayafuata yale aliyosema huyu mama basi tutafanikiwa kwa kiasi kikubwa kukomesha kabisa mauaji ya ndugu zetu hawa jamani.Tukumbuke kuwa thamaniya binadamu haiwezi kufananishwa na kitu chochote kile.Asante.