Friday, February 20, 2009

KILA LAHERI TAIFA STARS IVORY COAST.

Taifa Stars,sisi Watanzania wote tupo pamoja nanyi katika safari yenu ya kuliwania kombe la Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za ndani.Tunawaombea kila laheri ili muweze kuliwakilisha vema Taifa letu katika michuano hiyo mipya kabisa katika medani ya soka katika Afrika.Tulio wengi tunaamini kuwa mnaweza maana mpaka kufika hatua hiyo kwa kweli safari ilikuwa ndefu sana.
Kitu muhimu tunachowakumbusha watanzania wenzetu ni kuwa kwa kweli lazima muelewe kuwa huko mmekwenda kuwakilisha Taifa hivyo kwa njia moja au nyingine mko vitani ingawa si vita vya vifaru na mizinga bali vitavya mchezo wa soka lakini hiyo ni vita.Jitahidini kadri ya uwezo wenu mpambane kadri ya ujuzi wenu wote mliopewa na mwalimu na huku mkijua kuwa watanzania wote wapo nyuma yenu.
Kitu muhimu ni ushindi ingawa tupo tayari kuyapokea matokeo yoyote yale.
TUNA UHAKIKA KUWA MNAWEZA MAANA MPAKA KUFIKIA HAPO MLIPO KAMA NILIVYOKWISHA SEMA NI KUW MMEONYESHA KUW NINYI MU WAZURI KAMA HAO WENGINE!
Nahodha Nsajigwa hakikisha kuwa timu yako chini ya uongozi wako ndani ya kiwanja inakuwa na nidhamu wakati wote wa mchezo!Kubishana na waamuzi bila sababu ya msingi hakutaweza kutusaidia hasa ikizingatiwa kuw waamuzi wao ndiyo watoa maamuzi ya mwisho hata kama wachezaji hawakubaliani nayo.Nimekutaja nahodha kuwa unawajibika kuongoza nidhamu hasa tukumbukapo matukio ya nyuma pale tunapolalamika hata kama mwamuzi amepotoka lakini hkuna sababu ya kubishana naye sana kwani matokeo yake ni kadi na hiyo itapunguza ngu ya timu ingawaje wakayi mwingine inakuwa kichocheo cha timu kupigana kwa nguvu hadi mwisho baada ya kuijikuta kuwa tupo pungufu.Tuache hasira tuzingatie nidhamu tuwe na umoja tucheze kwa pamoja kama timu kama msemo wetu wa kiswahili usemavyo kuw umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu!
Tuna hakika kuwa viongozi wenu wamewaeleza na kuwajulisha majukumu yenu na mipaka yenu.
Hakika STARS KAMA MKIAMUA NA NINADHANI HIVYO KUWA MUMEAMUA BASI MTAWEZA NA INSHALAH KOMBE LITATUA KATIKA ARDHI HII YA BONGO!BRAVO TAIFA STARS ALUTA KONTINUA!TUPO PAMOJA NANYI.MUNGU IBARIKI TANZANIA MUNGU IBARIKI TAIFA STARS.

No comments: