Saturday, September 29, 2007

MASHAMBA YA MIWA YA MTIBWA!

Mtibwa Sukari ni eneo linalotoa picha ya kuvutia sana,upande wa mashariki wa eneo hilo limezungukwa na mashamba takribani ekari elfu nne za miwa,kota za wafanyakazi,kiwanda chenyewe cha sukari,miji midogo ya Mabau,Kidudwe,Mji unaokuja kwa kasi wa Madizini,hospitali ya Bwagala,mji wa Turiani mji wa Lusanga pamoja na shule yake maarufu ya sekondari ya Lusanga,chuo cha ualimu Muhonda na maeneo mengine mengi mazuri na ya kupendeza kama Kanga,Dihinda,Kwewmtonga,Mwenvuge,Divumbasa,Mlaguzi Chazi,Kigugu,Mbogo[Mtego wa Simba] Mkindo,Diongoya,Sungaji na maeneo mengi ya kuvutia bial kusahau milima tulivu na inayovutia milima ya Nguu.Kwa kweli maeneo haya yanatoa picha ya kupendeza sana.
Huko kuna timu ya mpira wa miguu ya Mtibwa Sukari ni eneo zuri na tulivu sana lakini kama unafika kwa mara ya kwanzxa unaweza ukataka kurudi leoleo!waja leo warudi leo lakini ukikaa kw siku kadhaa hutatamani kuondoka!Ardhi ina rutuba hali ya hewa nzuri maeneo yanavutia jinsi kulivyo ni kama tukichukua mtaa mmoja wa Dar acha tuseme kama Siza vile ndivyo kunavyofanana mahala pale.Nimewahi kuishi kule hususan maeneo ya Chazi Hospitali na nimekuwa na ndoto ya kuishi maeneo yale kwa maana yananivutia sana.Hata Salome Ihembe a.ka. Salome Leng'alwa analitambua hilo.Tukijaaliwa katika siku za usoni ninapenda sana kuhamishia makazi yangu huko,Turiani,Chazi,Mtibwa na maeneo ya jirani kwa kweli kwangu mimi yanatoa picha ya kupendeza sana.Salome upo!Mtibwa Sukari na hatima ya soka la Tanzania!Wasalimie Manungu!

No comments: