Saturday, September 29, 2007

SIMBA NA YANGA SI TIMU KUBWA BALI TIMU KONGWE!

Makala ya aliyewahi kuwa kocha wa Simba na Y anga kwa nyakati tofauti Siller Said Mziray leo katika gazeti la Mwanaspoti yamenifurshisha sana, ameandika kuwa timu za Simba na Yanga si timu kubwa katika soka la Bongo bali ni timu kongwe tu nchini ukilinganisha na timu zingine zinazoshiriki ligi ya VodaCom.Kwa kweli ameeleza ukweli mtupu.Ni kama nilivyosema katika makala yangu mojawapo kuwa zile zama za kufikiria kuw Simba na Yanga kuwa wao ndo kila mwaka watakuwa wafalme wa soka katika nchi hii kwa kweli zimepitwa na wakati.Hapa lazima ieleweke kuwa hizi timu hazitofautiani sana kwa kiwango cha soka bali zinazidiana uwezo wa kimaslahi kutokana na kuwa timu hizi ni kongwe na zina wapenzi wengi,wafadhiri wengi na vitu kama hivyo lakini kuhusu soka au kiwango cha kucheza wala havipishani sana na ti.mu zingine zinazoshiriki ligi ya VidaCom.
Hongera Mziray umeongea ukweli mtupu hata kama wadau wengine hawatakubali.Lakini ni sawa kabisa kuwa Simba na Yanga ni wakongwe tu wa soka la Bongo na kamwe wsijindanganye kuwa ni timu kubwa.Timu kubwa hazina wala uwanja wa kufanyia mazoezi achilia mbali mechi,timu kubwa hazina hata utaratibu unaoeleweka kuhusu wachezaji wake na timu kwa ujumla,timu kubwa zinakimbiwa na makocha kila kukicha na mbaya zaidi wanakimbiwa hata na makocha wazalendo je kunani pale Simba na Yanga?Ni ubabaishaji na uswahili mkubwa ndo unatawala pale.Wale wote wanaohusika na majukumu ya timu mbili hizi lazima wasome alama za nyakati na wakubali mabadiliko haraka sana.Simba na Yanga sisi ni wapenzi,wanazi wenu wakubwa kubalini mabadiko hizi ni zama zingine vinginevyo mtakuwa mnarudi nyuma daima badala ya kuenda mbele.Jiulizeni timu kama ElMerreikh miaka michache nyuma ilikuwa timu ya kwaida lakini leo hii angalia jinsi ilivyo angalia jinsi inavyomlipa kocha wake angalia inavyochanja mbuga katika soka la Afrika ina wachezaji wa kulipwa mpaka kutokaBrazil na imepiga hatua sana jamani.SIMBA ,YANGA TUACHE UBABAISHAJI KATIKA SOKA TUKUBALI MABADILIKO ILI HIZI TIMU ZIWE ZENYE KUOGOPEWA NA KUHESHIMIWA HAPA AFRKA HIZI NI TIMU KUBWA JAMANI ACHENI KUZIDHARIRISHA NINYI WADAU NA ACHENI KUWA HAPO KWA MASIRAHI YENU BINAFSI MUWE HAPO KWA FAIDA NA MAENDELEO YA MPIRA WA NCHI HII JAMANI HAKUNA LISILOWEZEKANA KWANI WAO WAWEZE WANA NINI NA SISI TUSHINDWE TUNA NINI.WAKATI NI HUU!TWENDE TUJIANDIKISHE SASA!

No comments: