Friday, September 28, 2007

NIDHAMU YA KAZI.

Msondo ngoma baba ya muziki wana magoma kitakita wale jamaa kiboko kwa tunzi zao mbalimbali.Nyimbo kama "NIDHAMU YA KAZI" kwa kweli ni moja ya nyimbo zenye ujumbe mzuri sana kwa jamii.Maana kazi ndiyo msingi wa maendeleo,kama alivyowahi kusema Baba wa Taifa "Kazi ndiyo msingi wa maendeleo,nchi masikini haiwezi kuendelea kama inategemea fedha kuwa ndiyo msingi wa maendeleo,nchi masikini haiwezi kuendelea kama inategemea misaada kutoka nchi za nje"Maneno haya aliyasema wakati anafungua uwanja wa Mapinduzi[uwanja wa Sokoine]Mbeya.
Nidhamu ya kazi ni msingi wa mafanikio mema kazini
Viongozi na wafanyakazi lazima sote tuwe na nidhamu
Migogoro na migongano ya kazini ni ukosefu wa nidhamu
Viongozi pia wajibu wenu mkubwa ni kulinda heshima
N kudumisha nidhamu ya kazi
Haya yote ni rahisi kuapatikana iwapo tutatia maanani suala la nidhamu!

No comments: