Saturday, September 29, 2007

MSAFIRI KAFIRI!

Jumamosi leo wiki endi mapumziko kwa wengi wetu baada ya wiki nzima ya kuchakarika na kazi zinazotuhusu,watu ni wengi Kariakoo,Posta,mitaa ya Kisutu na kila kona ya jiji.Kila mtu anajaribu kupata kile kilichomtoa nyumbani mchana huu.Madukani ni mshikemshike sokoni Kariakoo ndo usiseme,mtaa wa Msimbazi ni balaa tupu kuna mabasi mawili yamekodishwa na wapenzi wa Simba wanaojiita matawi ya mpira pesa wanajinadi kuwaeleza abiria kuwa usafiri upo wa kwenda Mji kasoro bahari kushuhudia pambano la mpira kati ya Simba na timu ya Pan Afrian[Twiga] ya Kinondoni.
Napita katika maduka ya TV nataka kununua TV maana ligi ya Uingereza siku hizi tunaifaidi kupitia TV ya Taifa shukurani kwa Tido Mhando kuwezesha sisi walala hoi kuona mpira wa kweli.Wauzaji wote hakuna anayesema ukweli kila mtu anavutia kwake unajua kilichotokea nimeamua kuachana na manunuzi ya TV nitanunua ya mtumba lakini sizipendi kwa kuwa zinachangia kuchafua mazingira ya hapa Bongo maana kwa nini zije huku wakati huko kwao zimeishatumika kwa nini watuletee siosi?Basi sitanunua kabisa!Ukipita madukani wote wanauza wanatumia lugha nzuri sdana na wana nidhasmu ya hali ya juu huwezi amini.Kweli sasa hivi Bongo biashara ni biashara huria!
Nimechoka kuzunguka madukani nipo Rik Pub nyuma ya jengo la Washirika nimeagiza msosi unapigwa wiombo wa Msafiri Kafiri navutiwa nao maana mimi ni penzi wa Msondo si unakumbuka jana nimeelezea kuhusu wimbo wa Msondo wa Nidhamu ya Kazi?
Hapa unapigwa Msafiri Kafiri kwa kweli nimechanganyikiwa mimi ni Mnazi mkubwa sana wa Msondo:
Msafiri kafiri mwenda pole hajikwai akijikwaa haumii kuumia kwake kidogo tuu
Mimi msafiri kafiri nakuja nawapisha wale waendao na warudio kwa haraka mimi naja taratibu!Msondo NGOMA YA wATANZANIA!WANACHEZEA UMEME HAO WATANASA SASA HIVI!

No comments: