Monday, September 24, 2007

SHULE YA MSINGI KIGUGU.

Shule ya msingi Kigugu ndiyo shule yangu ya kwanza kabisa 1976 mdogo kabisa miaka sita siku ya kwanza kwenda shule nililia sana naamshwa kwenda shule sitaki kisa mimi mdogo kwa nini niende shule?SHULE YETU!Unajua darasa lilipokuwa chini ya mwembe mwalimu wangu wa kwanza kunifundisha mwalimu Magdalena Ngwego tunaanza kwa kuandika chini au kuchora chini njaa inaniuma naamua kutoroka nakutana na akina mama wamepita maeneo ya shule naambiwa ahaa unatoroka shule tunaenda kukusemea kwa baba.Jamani tumetoka mbali lakini shule ni muhimu sana ila kufuatana na mazingira unayokuwa nayo wakati mwingine unaona kama ni jela ya sirisiri kama alivyowahi kuandika kwenye ukuta mwanafunzi mmoja kule Iyunga sekondari."Elimu ni ufunguo wa maisha"Nitaandika mengi sana kuhusu shule yangu ya kwanza ya msingi Kigugu Turiani,Morogoro.

No comments: